1. FASIHI YA KISWAHILI
KARATASI YA PILI
320/2
TAMTHILIA
Tamthilia ni nini?
• Tamthilia ni utanzu wa fasihi ambao huwasilishwa kupitia mazungumzo
na uigizaji ili kuwasilisha ujumbe wake. Kulingana na Wamitila (2007)
huu ni utanzu ambao huandikwa kwa mtindo wa mazungumzo ya
wahusika.
• Nkwera (h.t) anaelezea kuwa tamthilia ni: “Tamthilia ni mchezo wa
kuigiza au utungo wa kisanaa ambao huweka wazo fulani katika
matendo na mazungumzo” (Nkwera, h.t)
• Tamthilia (pia: Tamthiliya au Tamthilia-Mchezo) ni moja kati ya
sehemu ya utunzi wa hadithi au fasihi simulizi (ngano au hadithi)
ambayo mara nyingi tunaona kupitia katika makumbi au televisheni,
kusikia kupitia katika redio.
• Tamthilia au mchezo mara nyingi huwa mazunguzo baina ya watu, na
kwa kawaida huwa mchezo hatuutizami katika TV tu, bali hata kuna
watu wengine hufuatilia kwa kupitia maandiko yenye tamthiliya hizo
na kuzielewa vyema.
• Watu tunaowaona wanafanya tamthilia ni waigizaji; katika ukumbi
wa maonyesho husimama juu ya jukwaa na kuanza kutoa burudani
huku watu wakiwaangalia (watazamaji) wanaweza wakawaona vyema
kabisa.
• Mwongozaji ana wasaidia waigizaji waigizaji kufanya kazi zao vyema,
au anawaeleza namna ya mchezo jinsi vile unavyotakiwa kuchezwa.
AINA ZA TAMTHILIA
Kuna aina nyingi ya michezo au tamthiliya, kama vile;
1. Tamthilia Cheshi/Komedia - ni mchezo wa kuchekesha. Maudhui
yake huundwa kwa lengo la kutumbuiza hadhira.
2. Tamthilia Simanzi/Trejedia - ni mchezo uliojaa huzuni, mikasa,
mikosi, visa vya kutisha na aghalabu baadhi ya wahusika wakuu hufa.
1
2. 3. Tamthilia Simanzi-Cheshi/Trejikomedia - ni mchezo wenye visa
vya kuhuzunisha lakini pia unawasilisha kwa njia ya kuchekesha.
Aghalabu wahusika hutumia kejeli kuchekesha hadhira ijapokuwa kuna
shida fulani inayowakabili. Baadhi ya wahusika wakuu hukumbwa na
mikasa.
Mfano: Kifo Kisimani (na Kithaka Wa Mberia)
4. Tamthilia Tatizo - ni mchezo wa kuigiza ambapo wahusika huwa na
tatizo/shida kuu wanalotaka kulitatua. Tamthilia hii aghalabu hutumia
mbinu ya taharuki ili kuwafanya hadhira wawe makini ili kuona jinsi
tatizo hilo litakavyoishia.
5. Tamthilia ya Domestiki Drama - ni mchezo unaoangazia maisha
ya kawaida ya watu kama vile familia, urafiki, ndoa n.k
6. Tamthilia ya Melodrama - ni mchezo ambao husisitiza sifa za
wahusika kwa kuunda wahusika kuunda wahusika wenye sifa
zilizopigiwa chuku na zisizobadilika. Tamthilia hizi huundwa kwa
namna inayowafanya hadhira wawapende wahusika fulani na
wawachukie wahusika wengine. Kwa mfano:
• Shujaa ambaye hushinda kila mara.
• Wahusika wabaya ambao hubakia wabaya kutoka mwanzo
hadi mwishi.
• Wahusika wazuri ambao hufanya vitendo vizuri kutoka
mwanzo hadi mwisho.
• Wapenzi ambao hata wakitenganishwa bado watapendana
• Aghalabu huishia kwa raha mustarehe.
7. Tamthilia Tanzia /Trejidia - huu ni mchezo wa huzuni tu, kwa
sababu ya mikosi na nuksi iliyomo. Mara nyingi aina ya tamthilia hii
huwa na mwisho mbaya au wa huzuni na wenye kutisha sana.
MAUDHUI YA TAMTHILIA
Maudhui ya tamthilia yanagusia vipengele vya: migogoro, ujumbe,
falsafa, mtazamo, msimamo, na dhamira.
DHAMIRA YA TAMTHILIA
Matumizi ya tamthilia ni pamoja na: kuelimisha jamii; (katika masuala
mbalimbali kama vile: uchumi, siasa, maadili, nk.) kuburudisha jamii,
kuonya na kukosoa jamii, kukuza lugha, kurithisha amali za jamii (mila
na desturi za jamii husika), nk.
2